• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • MMM
    • Barua pepe za Watumishi
Local Government Loans Board

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Makatibu Waliowahi Kuongoza Bodi
    • Orodha ya Wajumbe wa Bodi
    • Orodha ya Mawaziri TAMISEMI
  • Huduma
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Kanuni
    • Kuomba Mkopo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Miradi
    • Miradi iliyokwisha
    • Mwongozo wa Uombaji wa Mkopo

Waziri Jafo Aitaka Mikoa Kusimamia Lishe Ili Kupunguza Udumavu

Posted on: December 20th, 2017

Waziri Jafo Aitaka Mikoa Kusimamia Lishe Ili Kupunguza Udumavu

Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe. Selemani Jafo (Mb) amewaongoza wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara, kupitia na kusaini Mkataba wa Utendaji kazi na Usimamizi wa shughuli za Lishe kwa kila mkoa katika kikao kazi kilichofanyika mjini Dodoma na kuwaomba wakasimamie suala la Lishe kwa nguvu zote.

Akiongea na Wakuu wa Mikoa katika ofisi za Wizara hiyo mjini Dodoma, Mhe. Jafo amesema maelekezo hayo awali, yalitolewa na Mhe. Makamu wa Rais wa Tanzania Mama Samia Suluhu, kuhusu tatizo la Lishe katika Mikoa na Kwa sasa Taifa limeamua kulishughulikia na Fedha imetengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018.

“Tumesaini hii mikataba kwa lengo kubwa la kuhakikisha kwamba Wakuu wa Mikoa kama viongozi wa Wakuu wa Mikoa, wahakikishe halmashauri zao zinaenda kutekeleza mipango yao ya bajeti ambayo imetengwa katika halmashauri zao hususan ni suala la Lishe ambalo kwa sasa ni agenda kubwa na tutataka tuisimamie ili kuondoa Udumavu katika jamii zetu.

Mhe. Jafo amesema Wakuu wa Mikoa wanayo dhamana kubwa ya kusimamia miradi ya maendeleo kama ujenzi wa vituo vya afya na suala la lishe kwa ujumla, hivyo Watendaji watoe taarifa zao kwa Wakuu wa Wilaya kabla ya kuwasilishwa kwa Wakuu wa Mikoa kwa hatua stahiki.


“Wakurugenzi watoe taarifa kwa Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Wilaya nao wawasilishe kwa Wakuu wa Mikoa ili waone namna ya kuzisemea taarifa hizo katika suala zima la utekelezaji wa mipango ya Serikali”.

Aidha, amewataka Wakuu wa Mikoa kuwaelekeza na kuwasimamia Wakurugenzi wa Halmashauri kwa ajili ya masuala ya lishe na ujenzi wa vituo vya afya 2011 ambavyo mpaka sasa vimeboreshwa na kujengwa ili kutoa huduma bora kwa jamii.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe S. Kebwe amesema, anaipongeza Serikali kwa kutoa takribani shilingi 11.6 Bilioni kwa ajili ya suala la lishe hasa katika kipengele cha udumavu.

Aidha, amesema suala zima la upatikanaji wa chakula mkoani Morogoro sio tatizo bali ni elimu ya ulaji chakula ndiyo inapaswa kutolewa ili kupunguza utapiamlo lakini pia kumekuwepo na tatizo la Maafisa Lishe katika halmashauri nchini kupangiwa kazi nyingine, kwa mfano kufanya kazi ya Idara tofauti kama vile kukusanya kodi.

Naye Stephen Motambi, Kaimu Mkurugenzi anayeshughulikia masuala ya Lishe Ofisi ya Rais TAMISEMI, amesema suala la Lishe limekuwa likifanyika katika Mikoa na Halmashauri zote katika kukabiliana na tatizo hili lakini kwa hivi sasa hali ya udumavu ni asilimia 34 hivyo mikoa inapaswa kuweka mikakati kuhusiana na kuondoa kabisa tatizo la lishe.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU WAHITIMU WA KIDATO CHA NNE,2023 KUFANYA MABADILIKO YA TAHASUSI ZA KIDATO CHA TANO NA KOZI ZA VYUO KWA MWAKA 2024 March 20, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA UANDISHI BORA WA MAANDIKO YA MIRADI ILI KUZIWEZESHA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA KUPATA PESA ZA MIRADI YA KIMKAKATI

    March 08, 2024
  • MAANDIKO BORA KUZIWEZESHA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA KUPATIWA MIKOPO KWENYE TAASISI ZA FEDHA

    March 25, 2024
  • LAAC: HATUTAKUBALI SERIKALI IPATE HASARA

    March 21, 2024
  • HALMASHAURI ZATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KUKOPA MIRADI MIDOGO

    March 13, 2024
  • Angalia Zote

Wasiliana Nasi

Local Government Loans Board

Sanduku la Barua: P.O Box 2710

Simu: +255 26 2321730

Barua Pepe: barua@lglb.go.tz

Fax:

Viungo vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • President's Office, Regional Adminstration and Local Government
  • MATUKIO

Zinazohusiana

  • Chuo cha Serikali za Mitaa
  • OR-TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI BLOG
  • Benki ya Maendeleo (TIB)

Video Mpya

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Miliki@ Bodi ya Mikoya Mikopo ya Serikali za Mitaa