• Malalamiko
    • Wasiliana Nasi
    • MMM
    • Barua pepe za Watumishi
Local Government Loans Board

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bodi ya Mikopo ya Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Makatibu Waliowahi Kuongoza Bodi
    • Orodha ya Wajumbe wa Bodi
    • Orodha ya Mawaziri TAMISEMI
  • Huduma
    • Huduma Zetu
  • Utawala
    • Muundo
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Kanuni
    • Kuomba Mkopo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
  • Miradi
    • Miradi iliyokwisha
    • Mwongozo wa Uombaji wa Mkopo

RAIS SAMIA AIWEZESHA REA BILIONI 96.8 UTEKELEZAJI MIRADI YA UMEME VIJIJINI DODOMA

13 May 2025

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa jumla ya kiasi cha shilingi bilioni 96.8 ili kuhakikisha miradi ya umeme vijijini inatekelezwa katika mkoa wa Dodoma na wananchi wanapatiwa huduma ya umeme ili kuwapatia maendeleo ya kiuchumi na kijamii

Hayo yamebainishwa Aprili 12, 2025 na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga wakati wa uzinduzi wa mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji 15 (HEP IIA) katika jimbo la Mvumi mkoa wa Dodoma

Mhe. Kapinga amesema, REA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali pamoja na kuwasimamia kwa karibu wakandarasi wote waliopewa zabuni ya kutekeleza miradi ilikuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliopangwa ili iweze kuwanufaisha wananchi.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Mvumi, Mhe. Livingstone Joseph Lusinde amesemaMwaka 2010 umeme ulikua kwenye vijiji viwili pekee lakini sasa vijiji vyote 60 vimefikiwa na huduma ya umeme na kuwaongezea chachu ya kufanya maendeleo wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja ameipongea REA kwa kuendelea kutekeleza miradi ya umeme vijijini ambayo imekuwa chachu ya maendeleo mkoani Dodoma.

Naye, Mkurugenzi wa Umeme Vijijini Mha. Jones Olotu amesema kuwa, Mkoa wa Dodoma una jumla ya vijiji 580 ambapo vijiji vyote sawa na asilimia 100 vimepata huduma ya umeme kupitia miradi ya awali kama vile REA awamu ya kwanza (REA I), REA awamu ya pili (REA II), REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza (REA III Round I), na REA awamu ya tatu mzunguko wa pili (REA III Round II).

"Jumla ya vitongoji 1,773 na mitaa 225 vimefikiwa na huduma ya umeme kati ya vitongoji 3,212 na mitaa 258 ya mkoa wa Dodoma ikiwa ni sawa na asilimia 57 ya vitongoji vyote, " Amesema Mha. Olotu

Mha. Olotu ameongeza kuwa, Wakala unaendelea na utekelezaji wa mradi waHEPIIA katika vitongoji 150 vya mkoa wa Dodoma kupitia mkandarasi Derm Group Ltd ambapo hadi kufikia mwezi March 2025, mkandarasi amekwisha kusimamisha nguzo katika vitongoji vyote.

Matangazo

  • RAIS SAMIA AIWEZESHA REA BILIONI 96.8 UTEKELEZAJI MIRADI YA UMEME VIJIJINI DODOMA May 13, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU WAHITIMU WA KIDATO CHA NNE,2023 KUFANYA MABADILIKO YA TAHASUSI ZA KIDATO CHA TANO NA KOZI ZA VYUO KWA MWAKA 2024 March 20, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MWENENDO WA UREJESHAJI MIKOPO KWENYE HALMASHAURI UNARIDHISHA - DKT. FESTO DUGANGE.

    May 08, 2025
  • MAFUNZO YA UANDISHI BORA WA MAANDIKO YA MIRADI ILI KUZIWEZESHA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA KUPATA PESA ZA MIRADI YA KIMKAKATI

    March 08, 2024
  • MAANDIKO BORA KUZIWEZESHA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA KUPATIWA MIKOPO KWENYE TAASISI ZA FEDHA

    March 25, 2024
  • LAAC: HATUTAKUBALI SERIKALI IPATE HASARA

    March 21, 2024
  • Angalia Zote

Wasiliana Nasi

Local Government Loans Board

Sanduku la Barua: P.O Box 2710

Simu: +255 26 2321730

Barua Pepe: barua@lglb.go.tz

Fax:

Viungo vya Haraka

  • Watumishi Portal
  • President's Office, Regional Adminstration and Local Government
  • MATUKIO

Zinazohusiana

  • Chuo cha Serikali za Mitaa
  • OR-TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • TAMISEMI BLOG
  • Benki ya Maendeleo (TIB)

Video Mpya

More Videos
    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Miliki@ Bodi ya Mikoya Mikopo ya Serikali za Mitaa